Jumanne, 7 Julai 2015

TABIA ZA VITENZI VYA KISWAHILI

  • Vitenzi vya Kiswahili huwa na tabia tofauti tofauti zinazotokana na dhima za mofimu ambazo hupachikwa katika vitenzi hivyo, hivyo kulingana na dhima za mofimu, vitenzi vya Kiswahili huwa na tabia zifuatazo:-
   I.               Kutambulisha nafsi. Mfano:- Anayesoma
    II.            Kutambulisha tendo. Mfano:- Cheza, Lima, Imba n.k.
III.            Kutambulisha wakati. Mfano:- Ulikuja 
 IV.            Kutambulisha hali ya uyakinishi na ukanushi. Mfano:- Anacheka – Hacheki 
   V.            Kutambulisha kauli mbalimbali za tendo. Mfano:- cheza-chezwa-chezewa-chezeka n.k.
VI.            Kutambulisha hali za nakati katika tendo. Mfano:-Huimba, Amekula. 
VII.            Kuonesha urejeshi wa mtenda, mtendwa na mtendewa ambao hujidhihirisha katika ngeli ya nomino iliyotajwa kwa kuzingatia upatanisho wa kisarufi. Urejeshi huo ni wa O-rejeshi. Katika urejeshi huo vitenzi hubeba viambishi ngeli vya –O- isipokuwa kama nomino ni ya ngeli ya kwanza umoja  ambapo hutumia –e- badala ya –O-.
Mfano:-
NGELI
KIAMBISHI CHA O- REJESHI
MFANO
A-WA
-YE- na –O-
Aliyepiga / Waliokuja
U-I
-O- na –YO-
Uliokatwa / Iliyokatwa
LI-YA
-LO- na –YO-
Lililochanika / Yaliyochanika
KI-VI
-CHO- na –VYO-
Kilichovunjika / Vilivyovunjika
I-ZI
-YO- na –ZO-
Iliyofungwa / Zilizofungwa
U-ZI
-O- na -ZO
Uliokatika / Zilizokatika
U-YA
-O- na –ZO-
Ulionipata / Yaliyonipata
KU
-KO-
Kulikotokea
PA-MU-KU
PO-MO-KO
Pale alipoingia / Mule alimotokea / Kule alikofunga

Maoni 17 :