Ni kipashio cha lugha
ambacho huwa na muundo wa neno moja au zaidi lakini huwa hakina muundo wa kiima
na kiarifu. Muundo wa kirai huwa ni wa neno moja au zaidi ambayo huwa pamoja
katika mpangilio maalumu wenye kuzingatia uhusiano wa maneno hayo na neno kuu
ambalo ndio huwa linabeba aina ya kundi hilo la maneno.
AINA ZA VIRAI
A. Kirai nomino (KN)
Hili ni kundi la
maneno ambalo hutawaliwa na nomino. Kirai nomino huundwa na maneno yafuatayo:-
o
Nomino pekee. Mfano; Asha
anapika, Nyangoye anaimba, Nyegera anacheza (N)
o
Nomino mbili au zaidi zinazounganishwa.
Mfano; Mhindi na Sagati wanacheza. (N+U+N)
o
Nomino na kivumishi. Mfano; Mtoto
mnene amekuja, Mzee mfupi ameondoka. (N+V)
o
Kiwakilishi pekee. Mfano; Yule
ameondoka, Wewe umenena, Wale waliokuja. (W)
o
Kiwakilishi na kivumishi. Mfano; Yule
mvivu amerudi, Wewe mlemavu njoo. (W+V)
o
Nomino na kitenzi jina. Mfano; Mchezo
wa kusisimua, Wimbo wa kupendeza. (N+Ktj)
o
Nomino na kishazi tegemezi kivumishi.
Mfano; Mjukuu aliyepotea, Mheshimiwa aliyeondoka. (N+βV)
B. Kirai kivumishi (KV)
Hiki
ni kirai ambacho muundo wake umejikita katika kivumishi na maneno yanayohusiana
na kivumishi katika tungo tungo hiyo. Virai hivi kwa kawaida hujibainisha zaidi
kimuundo kama sehemu ya virai nomino. Virai hivi huundwa na:-
o
Kivumishi na Kirai nomino. Mfano; Mwenye
mali nyingi, Wenye watoto wengi.
o
Kivumishi na kielezi. Mfano; Mzuri sana,
Mweupe
pee!,Mweusi tii!, Mbaya sana.
o
Kivumishi na kirai kitenzi. Mfano; Mwenye
kupiga gitaa, Mwenye kupenda sana.
o
Kivumishi na kirai kiunganishi. Mfano; Nzuri
ya kupendeza, Mpungufu wa akili.
C. Kirai kitenzi (KT)
Ni
kirai ambacho kimekitwa katika kitenzi, au katika uhusiano wa kitenzi na neno
au mafungu ya mengine ya maneno. Hii ina maana kwamba, neno kuu katika kirai
hiki ni kitenzi. Kirai kitenzi kimeundwa na vipashio vifuatavyo:-
o
Kitenzi pekee. Mfano; amekuja,
amekula,
ameoga.
(T)
o
Kitenzi kisaidizi na kitenzi kikuu.
Mfano; Alikua anacheza(Ts+T), Alikua anaweza kuimba. (Ts+Ts+T)
o
Kitenzi kishirikishi na shamirisho.
Mfano; Ni mtanashati, Ndiye mwizi, Sio mwelewa. (t+sh)
o
Kitenzi, jina na kielezi. Mfano; Nimepika
uji asubuhi
D. Kirai kielezi
Tofauti
na aina nyingine ya virai, miundo ya virai vielezi haielekei kukitwa kwenye
mahusiano ya lazima baina ya neno kuu (yaani kielezi ) na neno au fungu la
maneno linaloandamana nalo. Badala yake miuundo inayohusika hapa ni ya maneno
ambayo hufanya kazi pamoja katika Lugha kama misemo, neno au maneno yanayofuata
neno lililotangulia yakifafanua zaidi neno hilo. Zaidi kirai kielezi huelezea
namna, wakati, mahali na kinachofanya tendo hilo litendeke. Mfano; Mara nyingi,
Sana sana, Polepole, Jana asubuhi, Kesho mchana, n.k.
E. Kirai kihusishi
Ni
kirai ambacho muundo wake umekitwa katika mahusiano baina ya vihusishikwa, na,
katika,au kwenye na fungu la maneno linaloandamana nacho. Kwa maneno
menginekirai hicho ni kile ambacho neno kuu ni kihusishi. Virai vihusishi
japokuwa muundo wake hufanana ila hutofautiana kimaana, zipo maana tatuambazo
ni:-
a)
Pahala – kwa baba, katika kabati, kwenye
lindo
b)
Utumizi – Kwa kisu, Kwa mkono
Vilvile
kirai kihusishi hutumiwa kutekeleza majukumu yafuatayo katika sentensi:-
ü Kama
kivumishi. Mfano; Penseli ya mjomba, Mkoba
wa mama, Koti la babu
ü Kama
kielezi. Mfano; Tulisikiliza kwa makini,
Tuliimba kwa shangwe, Tulisoma kwa juhudi
ü Kama
kiwakilishi. Mfano; La mjomba
limetupwa, Ya shangazi imeuzwa, Wa nne ameondoka
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni