Jumanne, 7 Julai 2015

FASIHI KWA UJUMLA



                                                                      
1.      Nini maana ya fasihi? Bainisha tanzu na dhima za Fasihi.

  •  Swali hili linamhitaji mwanafunzi aeleze maana ya fashi kisha ataje na kueleza aina mbili za fasihi yaani Andishi na Simulizi na amalize kwa kueleza umuhimu wa fasihi kwa ujumla wake. Hivyo linaweza kujibika kama ifuatavyo:-

Fasihi ni sanaa ya kutumia lugha ili kuwakilisha wazo Fulani kwa hadhira kusudiwa. Sanaa ni ufundi wa kipekee unaokusudia kufanya kitu Fulani kivutie na kupendeza machoni mwa watu. Hivyo tunaposema kuwa fasihi ni sanaa ya lugha ina maana kuwa fasihi huipamba lugha ya kawaida kuonekana isiyo ya kawaida ili kuwavutia watu na kuwakosha kihisia. Si kila mtu anaweza kuwa msanii wa fasihi hivyo huwa kama tunu kwa mtu yaani kipaji.
Fasihi imegawanyika katika tanzu kuu mbili:-
i.                    Fasihi Simulizi. Utanzu huu wa fasihi ulianza tangu kuwepo kwa mwanadamu. Mwanadamu asingeweza kuishi vyema katika mazingira yake kijamii bila kuwasiliana, na ili kuwasiliana alihitaji lugha. Lugha ilitumika pia katika maburudisho mbalimbali na huo ndio ukawa mwanzo wa fasihi pia. Hivyo utanzu huu wa fasi ulianza tangu kuwepo kwa mwanadamu. Utanzu huu hutumia lugha ya masimulizi katika kufikisha ujumbe wake kwa hadhira kusudiwa. Kwa kusema hivyo kumbe; Fasihi simulizi ni utanzu wa fasihi utumiao lugha ya masimulizi ya mdomo kujikamilisha kidhima.
ii.                  Fasihi Andishi. Utanzu huu ulianza baada ya mwanadamu kuvumbua alama zinazowakilisha sauti za lugha yake. Alama hizo hujulikana kama andishi. Maandishi ni alama zinazowakilisha maumbo ya sauti ya mwanadamu. Kila lugha ina alama zinazowakilisha sauti za lugha hiyo. Hivyo utanzu huu ulikuja baada ya utanzu wa fasihi simulizi kuwepo. Fasihi andishi ni utanzu utumiaolugha ya maandishi kufikisha ujumbe kwa hadhira kusudiwa.
- Fasihi huwa na kazi mbalimbali katika jamii. Na zifuatazo ni miongoni mwa kazi nyingi za fasihi katika jamii, lakini lazima izingatiwe kuwa fasihi hulenga kufikisha wazo Fulani la msanii kwa hadhira kusudiwa hivyo wazo hilo linaweza kuwa la:-
Kuonya na kuadilisha jamii. Fasihi ina kazi ya kufichua mabaya na mazuri yanayotendeka katika jamii husika na haihishii hapo lakini pia hutoa maonyo juu ya mabaya hayo na zaidi kusifia na kuendeleza mazuri yote yaliyopo katika jamii husika, lengo ni kuimarisha utamaduni na maadili katika jamii. Iwapo watajitokeza watu Fulani wanaoenda kinyume na matakwa ya jamii, fasihi ina wajibu wa kuwasema waziwazi na kuwaonya juu ya mienendo yao huku ikiwarekebisha kifikra pia.
Kuelimisha jamii. Fasihi inalo jukumu la kutoa mafunzo mbalimbali kwa jamii. Mafunzo yanayorekebisha tabia na kudumisha utamaduni. Siku zote fasihi hulenga kuchunguza mambo yote yanayoendelea katika jamii mazuri na mabaya, kwa kuzingatia matukio ya kihistoria, hivyo huwa ni kazi ya waandishi na wasanii kuiandikia jamii ili kuelewa kile kinachoendelea ndani ya jamii kwa mapana na marefu ili asiwepo hata mwanajamii mmoja atakayekuwa nyuma ya wakati kwa kila matukio yanayojiri ndani ya jamii husika.
Kuwaburudisha wanajamii. Burudani ni hali ya kuamsha hisi za furaha za mwanadamu. Wasanii wengi hulenga suala hili. Ndivyo fasihi ilivyo, mtu huamishwa kihisia pale alipo na kufanywa kuwa kati8ka anga la furaha baada ya kusoma kazi ya fasihi. Msanii asiyefanikiwa katika suala hili basi inaaminika kuwa anayo mapungufu makubwa katika kazi yake na inajumuishwa kuwa hajafaulu kuiteka hadhira yake.
Kulinda na kuhifadhi amali za jamii husika. Utamaduni ni hali halisi ya maisha ya jamii Fulani, jumla ya imani katika mavazi yao, dini yao, lugha yao, miiko yao, maadili yao na desturi zao.  Hivyo fasihi huwa na kazi ya kulinda jumla hizo na kuziendeleza ili ziwepo vizazi hata vizazi.
Kudumisha na kuendeleza lugha. Fasihi hutegemea lugha kama zana ya kufikisha ujumbe kwa hadhira kusudiwa. Hivyo ni njia nzuri tu ya kukuza na kuimarisha lugha ya jamii husika kwa kuwa njia kuu ya uwasilishwaji wake ni lugha. Maneno mengi yanayotumiwa na wanajamii yana mwanzo wake kutoka kwa wasanii wa mashairi, riwaya, tamthiliya, nyimbo na hata sanaa za maonesho.
Hivyo ni wazi kuwa fasihi ina wajibu mkubwa sana katika jamii kama inavyodhihirishwa katika hoja hizo hapo juu. Lakini izingatiwe kuwa ili fasihi kuwa fasihi lazima iwe na sifa zifuatazo, iwe na ufundi, ufundi huo uwe wa lugha, lugha inayoelezea kinachotendeka  katika jamii na maelezo hayo yawe na fani na maudhui. Hizo ndizo sifa za Fasihi.




2.      Fasihi simulizi na Fasihi andishi hutofautiana kitanzu. Fafanua kauli hii.

  •   Swali hili linakusuduia mwanafunzi aweze kueleza bayana tanzu za fasihi simulizi na fashi andishi zinavyotofautiana.

Fasihi simulizi ni utanzu wa fasihi unaowasilisha ujumbe wake kwa njia ya masimulizi ya mdomo, ilhali fasihi andishi ni ule utanzu wa fasihi unaowasilishwa kwa njia ya maandishi katika machapisho.  Si uwasilishwaji tu unaoleta utofauti wa fasihi andishi na simulizi lakini pia tanzu zao hutofautiana. Zifuatazo kwanza ni tanzu za fasihi simulizi:-
Hadithi. Ni tungo za kifasihi zitumiazo lugha ya nathari. Lugha ya nathari ni lugha ya mjazo inayotumiwa katika matumizi ya kwaida ya kilan siku. Masimulizi hayo huwa yanakuwa katika mtiririko maalum unaokamilisha visa. Vipera vya Hadithi ni kama; Ngano – ambazo huwa ni hadithi za kimapokeo zitumiazo wahusika kama wanyama, mimea na watu kufikisha ujumbe, Vigano – huwa hadithi fupi zinazxolenga kuadilisha zaidi, Soga – ni hadithi fupi zinazolenga kukejeli na kuchekesha, Tarihi – husimulia matukio ya kihistoria yanayobuniwz au yale yaliyotokea kweli, na Visasili – ni hadithi zinazotumia wahusika mbalimbali kama watu na miungu.
Semi. Ni fungu la tungo la fasihi simulizi ambazo huwa ni fupifupi zinazotumia picha, tamathali za semi na ishara. Huwa na aina zifuatazo; Methali – hueleza kwa ufupi fikra au mafumbo yaliyomo kwenye fikra za mwanadamu, Vitendawili – ni usemi uliofumbwa ambao hutolewa ili ufumbuliwe, Nahau – ni misemo ya picha ambayo huleta maana iliyofichika, Misemo – ni fungu la maneno linalotumiwa na jamii ya watu kwa namna maalumu ili kutoa maana Fulani, Mizungu – ni kauli yenye picha za mafumbo na inayoonesha ukinzani wa fikra au tukio.
Ushairi. Ni fungu linalojumuisha tungo zote zenye mapigo ya kimuziki yaliyopangwa kwa utaratibu maalumu mathalani yakiwa yamepangwa kwa muwala wa urari. Ushairi huwa na aina hizi; Nyimbo – Ni kile kinachoimbwa yaani hali ya kupanda na kushuka kwa sauti kimuziki, Maghani – ni ushairi unaotolewa kwa kalmia badala ya kuimbwa, Ngonjera – huwa na muundo wa mashairi ya kimapokeo na hutumia lugha ya mazungumzo ya majibishano baina ya watu wawili au zaidi.
Sanaa za maonesho. Ni sanaa ambazo uzuri wake unajkitokeza katika umbo lakudumu ambalo huweza kuoneshwa muda wowote  kama vile uchongaji, uchoraji, udarizi, ufinyanzi n.k. Sanaa za maonesho hujitokeza kupitia; Matambiko – hii ni sanaa ya maoneshop ambayo huusisha utoaji wa sadaka zinazoelekezwa kwa Mungu, miungu, mizimu hata mapepo, Majigambo – ni snaa ya maonesho ambayo mtu hutoa masimulizi ya kujigamba kuhusu ushujaa wake nay ale aliyoyatenda maishani mwake, Miviga – ni sherehe zinazofanywa na jamii Fulani kwa lengo la kufundisha vijana na hufanyika katika kipindi maalumun kila mwaka, Ngoma – huusisha uchezeshaji nwa viungo vya mwili wenye kuzingatia upekee wa mdundo na miondoko maalumu.
Fasihi Andishi imepata tanzu zake kutokana na fasihi simulizi, kwa maana kwamba kila utanzu uliopo katika fasihi andishi una chimbuko lake katika fasihi simulizi sema tu umebadilishwa kwa kuwekwa katika mpangilio maalumu wa kimamaandisahi. Zifuatazo ni tanzu za fasihi Andishi:-
Riwaya. Riwaya imetokana na hadithi katika fasihi simulizi, hivyo ni hadithi ndefu zenye ubunaji ndani yake ambazo kwa mawanda mapana huwasilisha ujumbe wake kwa hadhira kwa kutumia lugha nathari ambayo huwa na mchangamano wa visa na matukio yanayomulika maisha halisi ya jamii husika.
Tamthiliya. Imetokana na sanaa za maonesho katika fasihi simulizi, ni utungo wa kimchezo wa kuigiza yaani drama ambao unawasilishwa kupitia maandishi. Tamthiliya huweza kuigizwa jukwaani kwani huandikwa kwa kudhihirisha matendo na majibizanon ya wahusika hivyo ina mtindo wa lugha ya majibizano yaani dailojia.
Ushairi. Huu umetokana na utanzu wa ushairi katika fasihi simulizi, ambapo ni sanaa inayopambanuliwa kwa mpangilio maalumu wa maneno fasaha na yenye mvuto, hutumia lugha ya mkato, na kunakuwa na matumizi ya lugha ya picha na ishara ili kueleza wazo, vilevile huweza kuimbika. Hivyo kutokana na hayo ushairi ni sanaa inayoambatana na kuibua hisia kutokana na ulimwengu ambyo hutumia lugha ya mkato na yenye urari kimuundo.
Kwa hiyo basi ni msingi tu kutambua kwamba tanzu mbili za fasihi yaani fasihi simulizi na fasihi andishi zinatofautiana kitanzu, kwa kuwa fasihi simulizi ina tanzu nne wakati fasihi andishi ina tanzu tatu, na pia fasihi andishi imezipata tanzu zake kutoka katika fasihi simulizi.
3.       Fafanua vigezo tofauti tofauti vinavyoleta utofauti katika tanzu mbili za fasihi.
v  Swali hili linamhitaji mwanafunzi wa kueleza tofauti ya fasihi andishi nan fasihi simulizi.
Fasihi ni sanaa itumiayo lugha katika kufikisha ujumbe kwa hadhira kusudiwa, ikiwa na tanzu mbili, tanzu hizo hutofautiana katika vipengele vifuatavyo kama inavyoonekana katika jedwali hili hapa chini:-
KIPENGELE
FASIHI SIMULIZI
FASIHI ANDISHI
1.      Umri
Ni kongwe kwa kua imeanza mara baada tu ya chimbuko la mwanadamu.
Ni matokeo ya fasihi simulizi, hivyo ni changa bado maana ni zao la fasihi simulizi.
2.      Uhifadhi
Uhifadhiwa kichwani kabla ya kuanza pia kuhifadhiwa katika vinasa sauti baada ya mabadiliko ya sayansi na tekinolojia.
Huifadhiwa katika maandishi.
3.      Uwasilishwaji
Huwasilishwa kwa masimulizi ya mdomo.
Huwasilishwa kwa njia ya maandishi.
4.      Umiliki
Ni mali ya jamii.
Ni mali ya msanii.
5.      Hadhira
Ni watu wote katika jamii
Ni wale wajuao kusoma pekee.
6.      Tanzu
Huwa na tanzu nne yaani; semi, hadithi, ushairi na sanaa za maonesho.
Huwa na tanzu tatu yaani; ushairi, tamthiliya na riwaya.

7.      Mabadiliko
Hubadilikia kwa haraka kulingana na mahitaji ya hadhira.
Hudumu katika hali ileile kwa muda murefu.
8.      Utendaji
Huambatana na utendaji.
Hakuna utendaji.









4.      Uhifadhi wa kazi ya fasihi simulizi umegawanyika katika njia tofauti tofauti, zielezee.

  • Swali hili linamhitaji mwanafunzi azielezee njia mbalimbali za kuhifadhi fasihi simulizi. Sweali hili linawezxa kujibika kwa mfumo ufuatao:-

Fasihi simulizi ni sanaa ya lugha inayowasilishwa kwa njia ya masimulizi yam domo. Fasihi simulizi ni moja kati ya tanzu mbili za fasihi na huu ndio utanzu mkongwe zaidi kuliko ule wa fasihi andishi. Fasihi simulizi huweza kukusanywa na kuhifadhiwa kupitia njia zifuatazo:-
Kichwa. Tangu awali, fasihi simulizi imekuwa ikihifadhiwa kichwani mwa fanani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya masimulizi ya mdomo. Hii imekuwepo tangu mwanzo fasihi ilipoanza na ndio sababu imekuwa ikirithishwa kizazi hata kizazi kupitia masimulizi hayo ya fanani kwenda kwa hadhira ambayo hutoka moja kwa moja katika chopmbo cha kuhifadhia yaani kichwa.
Kanda za kunasia sauti. Kutokana na maendeleo ya sayansi na tekinolojia fasihi simulizi imeweza kuhifadhiwa katika kanda za kunasia sauti, hii njia inasaidia fasihi kufikishwa kwa muda na mahali popote bila ya kuwepo na fanani hai.
Maandishi. Fasihi simulizi

Maoni 11 :

  1. fasihi simulizi huweza kupotea haraka kwa vile mara nyingi huhifadhiwa kwa kutumia kichwa.

    JibuFuta
  2. Je tofauti kati ua lugha ya kifasihi na lugha isiyo ya kifasihi ni ipi

    JibuFuta
  3. Tofauti kati ya lugha ya kifasihi na lugha isiyo yakifasihi

    JibuFuta
  4. Tofauti kati ya lugha ya kifasihi na lugha isiyo yakifasihi

    JibuFuta
  5. Naomba kujua chimbuko la fasihi

    JibuFuta
  6. Tanzu za fasihi andishi ni zao la fasihi simulizi.Thibitisha dai hili kwa mifano bayana

    JibuFuta
  7. kazi ya wizi weka marejeleo

    JibuFuta
  8. "Umuhimu wa kazi za fasihi, hutofautiana kutegemeana na utanzu husika" jadili hoja hii kwa kutumia tamthiliya na Riwaya.

    JibuFuta