Mofimu ni
kipashio kidogo kabisa cha lugha ambacho kina uwezo wa kusitiri maana ya neno
ambalo kwalo limeundwa. AU ni kipashio kidogo kabisa cha lugha chenye maana
kisarufi.
AINA ZA
MOFIMU
Mofimu huru ni
aina
ya mofimu ambayo huweza kusimama pekee na kujitosheleza kimaana yaani
huwa
na sifa ya neno. Mfano; mama, Baba, Dada, Kaka, Mjomba, Shangazi n.k.
Kwa mifano hiyo utagundua kuwa mofimu huru haziwezi kugawanyika zaidi na
kubeba maana
kisarufi, kwa maana kwamba mofimu ‘baba’ ikigawanywa ba-ba, ‘ba’ hii
haina
maana yoyote kisarufi zaidi ya kuwa silabi.
Mofimu tegemezi ni
aina ya mofimu ambayo huweza kuvunjwavunjwa na kubeba maana kisarufi, mofimu
tegemezi hutegemeana ili kuleta maana kamili ya neno.
Mfano;
neno ‘anakula’ limeundwa na mofimu zifuatazo:- [a-na-kul-a] ambazo kila moja
hubeba dhana Fulani ya kisarufi.
VIAMBISHI
Ni mofimu zinazopachikwa nyuma au
mbele ya mzizi wa neno ili kubadilisha dhana ya neno. Kwa kuwa mofimu hizo
hupachikwa sehemu tatu tofauti, tunapata aina tatu za viambishi kwa mujibu wa
nafasi zake katika neno, yaani; viambishi awali ambavyo hupachikwa mwanzoni
au nyuma ya mzizi wa neno,viambishi kati ambavyo hupachikwa katikati ya
neno (Kiswahili hakina viambishi hivi) na viambishi tamati ambavyo hivi
hupachikwa mbele au mwishoni mwa mzizi wa neno.
Mfano:-
VIAMBISHI
AWALI
|
MZIZI WA NENO
|
VIAMBISHI
TAMATI
|
NENO JIPYA
|
||
A
|
na
|
chez
|
ew
|
a
|
Anachezewa
|
Wa
|
li
|
chez
|
ean
|
a
|
Walichezeana
|
Tu
|
ta
|
chez
|
e
|
a
|
Tutachezea
|
1. Viambishi awali Hivi
hupachikwa kabla ya mzizi wa neno na huwa ni vya aina tisa:-
i.
Viambisha awali vya nafsi- hivi hudokeza
upatanishi wa nafsi katika kitenzi, zipo
nafsi tatu, nafsi ya kwanza, ya pili, naya tatu.
NAFSI
|
UMOJA
|
UWINGI
|
Ya Kwanza
|
Ni-
|
Tu-
|
Ya Pili
|
U-
|
M-
|
Ya Tatu
|
A-
|
Wa-
|
M
Mfano:-Ninalima
Tunacheza
ii.
Viambishi awali vya ngeli- hivi
hupatikana mwanzoni mwa nomino au vivumishi ili kudokeza hali ya umoja na
uwingi.
Mfano:-Mtu
(umoja) – Watu (uwingi)
Msafi (umoja) – Wasafi
(uwingi)
iii.
Viambishi awali vya ukanushi - hivi
hudokeza hali ya uhasi wa tendo. Huwakilishwa na mofimu (ha-) na (si-)
Mfano:- Amekula
(uyakinifu) – Hajala (ukanushi), Nakula (uyakinifu) – Sili
(ukanushi)
iv.
Viambishi awali vya Njeo- hivi hudokeza
nyakati mbalimbali ambazo ni wakati uliopita, uliopo na ujao.
NYAKATI
|
MOFIMU
|
Uliopo
|
-Na-
|
Uliopita
|
-li-
|
Ujao
|
-Ta-
|
Mfano:-
Mlituona
Utakuja
v.
Viambishi awali vya hali- hivi hudokeza
hali mbili za nyakati ambazo ni mazoea ambayo huwakilishwa na mofimu {hu} na
timilifu inayowakilishwa na mofimu {me}.
Mfano:-Hucheza
Amelima
vi.
Viambishi awali vya masharti-hivi
hudokeza hali ya masharti au uwezekano katika tendo. Mofimu hizo ni kama –ki-,
nge-, ngali- n.k.
Mfano:-
ukija
Ungekuja
Angalimkuta
vii.
Kiambishi cha urejeshi wa mtenda (kiima)-
mhiki hudokeza urejeshi wa nomino inayotenda katika kitenzi.
Mfano:
- Aliyekuja {-ye-} hudokeza urejeshi wa mtenda.
viii.
Kiambishi kiwakilishi cha mtendwa au
mtendewa (shamirisho) – hivi huwakilisha mtendwa au mtendewa wa jambo.
Mfano;
Nilimpiga,
Uliukata,
Nimeipenda,
Wameniteta.
ix.
Kiambishi awali cha kujirejea
(kujitendea) – hiki huwakilishwa na mofimu (-ji-)
Mfano;
kujipenda
2.
Viambishi
tamati– Hivi hudokeza kauli mbalimbali za vitenzi.
Mfano: - Anacheza –
kutenda
Unachezwa-
Kutendwa
Utachezewa- Kutendewa
Nimemlia- Kutendea
Wamewasomesha- Kutendesha n.k
Mzizi
|
Kiambishi cha
Kauli
|
Kiambishi
tamati maana
|
Neno jipya
|
Kauli
|
Viambishi
vya kauli
|
Chez
|
a
|
Cheza
|
Kutenda
|
-a
|
|
e
|
a
|
Chezea
|
kutendea
|
-e-
|
|
Pig
|
ian
|
a
|
Pigiana
|
Kutendeana
|
-ian-/-ean-
|
iw
|
a
|
Pigiwa
|
Kutendewa
|
-iw-/ew-
|
|
Som
|
esh
|
a
|
Somesha
|
Kutendesha
|
-ish-/esh-
|
eshw
|
a
|
Someshwa
|
Kutendeshwa
|
-ishw-/eshw-
|
|
Lim
|
ik
|
a
|
Limika
|
Kutendeka
|
-ik-/-ek-
|
an
|
a
|
Limana
|
Kutendana
|
-an-
|
|
w
|
a
|
Limwa
|
Kutendwa
|
-w-
|
DHANA YA MZIZI NA SHINA LA KITENZI
Mzizi
wakitenzini sehemu ya neno inayobakia mara baada
ya kuondoa viambishi vyote vya awali na tamati katika neno hilo. Mfano: -
a-na-chez-a {-chez-}, m-ku-lim-a {-lim-}
Mzizi
fungeni ule ambao hauwezi kujikamilisha kimaana yaani
hauwezi kusimama kama neno. Mfano; -lim-, -chez-, -imb- n.k.
Mzizi
huruni
ule ambao huweza kusimama kama neno na ukichanganuliwa zaidi hupoteza maana
yake ya msingi. Mfano; Kinu, Kazi, Arifu, Sali n.k.
Shina
la kitenzi ni sehemu ya neno ambayo huongezwa
viambishi fuatishi (tamati) au ni sehemu ya neno ambayo hubakia baada ya
kuondolewa viambishi tangulizi. Mfano:- chez+a = cheza, lim+a = lima. Sehemu
hii ya neno hutumika kuundia neno jipya.
Shina
sahili – hili ni shina ambalo huundwa na mofimu moja tu
ambayo ni mzizi wa neno hilo, huwa ni mofimu huru, Mfano; Kesho, jana, kitabu,
jarida n.k.
Shina
changamano – shina hili huundwa na mzizi na kiambishi tamati
maana. Mfano; cheka, lala, lia, kula n.k
Shina
ambatani – shina hili huundwa na mofimu mbili ambazo ni
huru. Mfano; mwana + kwenda = mwanakwenda, mbwa + mwitu = mbwamwitu
kongole
JibuFutaPongezi sana kwa Nazi yenu nzuri
JibuFutaPongezi sana ila dhima ndo zipi naomb kueleweshwa
JibuFutaHONGERA BWANA
JibuFutaNaomba kufahamishwa zaidi kuhusu maana ya kisarufi na kileksika
JibuFutaHongera kwa somo zuri
JibuFutaMe nahitaji dhima
JibuFutaSafi
JibuFuta