Ni namna ya kuweka majina katika makundi
yanayofanana. Majina ya Kiswahili yanaweza kuwekwa katika makundi mbalimbali.
Makundi hayo yamegawa na wanaisimu ya Kiswahili kwa kuzingatia maumbo ya
alomofu za umoja na uwingi wa majina (kimofolojia) na kwa kuzingatia namna
majina yanavyopatana na viambishi awali vya vitenzi (upatanisho wa kisarufi /
kisintaksia).
1.
Kimofolojia:
Katika
kigezo hiki wanaisimu wameyapanga majina kulingana na alomofu za umoja na
uwingi za majina hayo. Huu ni mtazamo mkongwe ambao uliofuatwa na wanasarufi wa
kimapokeo wakiongozwa na Meinholf, Broomfield na Ashton mnamo miaka ya 1920 –
50. Uchambuzi ulikua kama ifuatavyo:-
1.
M-
2.
WA-
|
i). Majina ya
viumbe vyenye uhai
ispokuwa
mimea. Mfano; Mtoto – Watoto, Mzee – Wazee, Mkurya - Wakurya
ii) Majina yanayotokana na vitenzi
vinavyotaja
watu. Mfano; Msomi – Wasomi, Mkulima – Wakulima, Mfanyakazi – Wafanyakazi.
|
3.
M-
4.
MI-
|
i). Majina ya mimea.
Mfano; Mti – Miti, Mwembe, Miembe, Mpera – Mipera.
ii) Majina ya vitu
yanayoanza na M- Mfano; Mto – Mito,
Msumari – Misumari.
|
5.
KI-
6.
VI-
|
i). Majina ya
vitu yanayoanza na ki- (umoja) na vi- (wingi). Mfano; Kiti – Viti, Kisu – Visu, Kikapu – Vikapu.
ii). Majina ya
viumbe yanayoambishwa na ch- umoja na vy-uwingi. Mfano; Chura – Vyura, Chakula – Vyakula, Chuma – Vyuma.
|
7.
JI-
8.
MA-
|
i).
Majina
yanayoanza na ji- umoja na ma- uwingi. Mfano; Jicho – Macho, Jini
– Majini, Jiwe – Mawe, Jina – Majina.
ii). Majina ya mkopo yenye ma- (wingi). Mfano; Bwana
– Mabwana, Shati – Mashati.
iii). Majina
yenye kueleza dhanna ya wingi japokuwa hayahesabiki. Maji, Majani, Maua,
Maini.
|
9.
N-
|
i). Majina ambayo huanza na N
inayofuatwa na konsonanti, ch-, d-,
g-, j-, z-, na
y- katika umoja na wingi. Mfano; Nchi, Ndama, Ngoma, Njaa, Nzi, Nyasi.
ii). Majina
yanayoanza na mb-, mv. Mfano; Mbwa, Mvi.
iii). Majina
ya mkopo. Mfano; Taa, redio, Kompyuta, Kalamu.
|
10. U-
11. N-
|
i).
Majina
yote yanayoanza na U umoja na N-, mb (wingi). Mfano; Ubao – Mbao, Ulimi
– Ndimi, Uso – Nyuso.
|
12. U-
13. MA-
|
i). Majina
yote yanayoanza na uumoja na ma- wingi. Mfano; Uasi – Maasi, Uchweo – Machweo, Ugonjwa – Magonjwa.
|
14. KU-
|
i). Majina
yanayotokana na vitenzi yanayoanza na ku- (vitenzi-jina). Mfano; kucheza,
Kulima, Kuimba, Kupenda.
|
15. PA-
|
i).
Huonesha mahali hasa. Mfano; Pale
|
16. MU-
|
i).
Huonesha mahali pa ndani. Mfano; Mule
|
17. KU
|
i).
Huonesha mahali pa mbali, pakubwa zaidi au popote. Mfano; Kule
|
UBORA
WA KIGEZO CHA KIMOFOLOJIA
I.
Uwezekano wa kuzigawa nomino nyingi za Kiswahili
ni mkubwa kwa kuwa nyingi zimegawanyika katika maumbo hayo ya umojha na uwingi.
II.
Ni kigezo muhimu kwani kinajikita zaidi
katika nomino na kivumishi chake peke yake hakigusi aina nyingine ya neno
tofauti na kigeso cha kisintaksia ambacho hugusa hadi kitenzi.
III.
Huwasaidia wanasarufi linganishi
kuonesha uhusiano wa lugha za vikoa kimoja.
UPUNGUFU WA KIGEZO HIKI.
I.
Kuna viambishi katika ngeli tofauti
vinavyofanana. Mfano Kiambishi M- kinajitokeza katika ngeli ya 1 na 3 na MA-
inajitokeza katika ngeli ya 8 na 13.
II.
Kuna nomino nyingine ambazo
hazijidhihirishi katika umoja na uwingi. Mfano ngeli ya 8 na 9.
2.
Kigezo cha sintaksia /upatanisho wa
kisarufi:
Huu ni mtazamo wa kisasa wa uainishaji wa
ngeli ambao umeyagawa majina katika makundi kulingana na upatanisho wa kisarufi
kat ya jina na viambishi awali vilivyo katika vitenzi. Kwa mujibu wa mtazamo
huu, majina yamepangwa katika makundi tisa ambayo ni:-
1. A -WA
Mfano;
Mtoto anacheza / Watoto wanacheza.
Mzee analima / Wazee wanalima.
Mwanafunzi anasoma / Wanafunzi wanasoma.
2.
U
– I
Mfano; Mkufu umekatika / Mikufu imekatika.
Mji umevamiwa
/ Miji imevamiwa.
Mkaa umemwagika / Mikaa imemwagika.
3.
LI
– YA
Mfano;
Gogo limevunjika / Magogo yamevunjika.
Gari limepotea / Magari yamepotea.
Jiko limewaka / Majiko yamewaka
4.
KI
– VI
Mfano;
Kiapo kimekiukwa / Viapo vimekiukwa.
Kilima kimesawazishwa / Vilima vimesawazishwa.
Kikongwe kimeuawa / Vikongwe vimeuawa.
5.
I
– ZI
Mfano; Ng’ombe imechinjwa / Ng’ombe zimechinjwa.
Nguo imechanika / Nguo zimechanika.
Nchi imekosa amani / Nchi zimekosa
amani.
6.
U
– ZI
Mfano; Ubao umeandikika / Mbao zimeandikika.
Ukuta umeanguka / Kuta zimeanguka.
Uzi umetumika
/ Nyuzi zimetumika.
7.
U
– YA
Mfano; Ugonjwa unatisha / Magonjwa yanatisha.
Uasi umekithiri / Maasi yamekithiri.
8.
KU
Mfano; Kulima kunachosha.
Kuimba kwake kunafurahisha.
Kufurahi kwake kumemponya.
9.
PA
– MU - KU
Mfano; Hapa pananuka.
Humu mna nzi.
Kule kumebomoka.
UBORA WA KIGEZO CHA
KISINTAKSIA
n Unajitosheleza
kwa kuwa kila jina inakuwa na upatanishi wake katika kitenzi.
UPUNGUFU WA KIGEZO HIKI
I.
Kuna viambishi vinavyojirudia. Mfano, U-
kimejitokeza katika ngeli ya 2, 6 na 7.
II.
Huyaweka majina yenye maumbo tofauti
katika ngeli moja.
III.
Kunaweza kuwa na utata katika upatanisho
kwa baadhi ya majina kama “makala”
Mfano;
Makala yamechapishwa.
Makala imechapishwa.
Sentensi hizo zote
zinatumika ila hatuna wingi wa makala katika Kiswahili
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni