1. KISHAZI
Ni
aina ya tungo ambayo huwa na kitenzi ndani yake, kitenzi hicho kinaweza kikawa
kinakamilisha maana au kisiwe kinajikamilisha kimaana. Kitenzi ambacho huwa
kinakamilisha maana huwa ni kitenzi kikuu (T), na kile kisichokuwa kinatoa
taarifa kamili huwa ni kitenzi kisaidizi (TS). Kwa mujibu huo tunapata aina
mbili za kishazi yaani kishazi huru
na kishazi tegemezi.
A.
Kishazi
huru (K/Hr)
Aina
hii ya kishazi huwa na tabia ya kutoa taarifa ambayo huwa ni kamili katika
tungo, hubeba kitenzi kikuu au kishirikishi ndani yake. Kishazi hiki huwa
hakihitaji maelezo ya ziada ili kukamilisha maana au taarifa kusudiwa na pia
huweza kujitegemea kama sentensi kamili na huwa na muundo wa kiima na kiarifu.
Mfano;
Mtoto / anacheza mpira
K A
Mwanafunzi / anasoma kitabu
K A
Mwanaume / anakufahamu
K A
Mwanafunzi /. ni mpole
K A
B. Kishazi tegemezi (K/ Tg)
Aina
hii ya kishazi huwa haitoi taarifa iliyokamili badala yake hutegemea kishazi
huru ili kukamilisha taarifa iliyokusudiwa na msemaji. Kishazi hiki hutawaliwa
na kitenzi kisaidizi. Kishazi tegemezi kwa upekee wake hakiwezi kutoa taarifa
iliyokusudiwa. Vishazi tegemezi hushuka hadhi na kuwa na hadhi ya kikundi cha
maneno (kirai).
Mfano; Mtoto unayemjua
Mwanafunzi anayesoma
Mahali alipoingia
Mama alipomchapa
Kaka aliporudi
Vishazi
hivyo hapo juu havitoi taarifa iliyokamili ila tunapoviweka pamoja na vishazi
huru taarifa iliyokusudiwa hukamilika. Tazama hapa chini:-
Mfano; Mtoto
unayemjua ameondoka
Mwanafunzi anayesoma atafaulu
Mahali alipoingia ni pachafu
Mama alipomchapa aliondoka
Kaka aliporudi alinifurahisha
Sifa za kishazi tegemezi
i.
Hakikamilishi taarifa pasipokuwepo na
kishazi huru
Mfano; Mtoto
anayecheza mpira ameumia
Mvulana aliyefaulu mtihani amefurahi
Mama
alipomkaribisha aliingia ndani
ii.
Kinaweza kuondolewa katika tungo bila
kuathiri taarifa kusudiwa.
Mfano; mtoto aliyeugua
amepona
Mtoto amepona
Mama uliyemsalimia pale ameondoka jana.
Mama ameondoka jana
iii.
Hutambulishwa na vitambulishi vya
urejeshi vinavyopachikwa katika vitenzi.
Mfano;
Anayesoma, Alichookota, Uliokatika, Iliyoibiwa, Alipoingia
n.k.
iv.
Vilevile kashazi tegemezi hutambulishwa
na viunganishi tegemezi kwamba, ili, ili kwamba, kwa sababu, mzizi wa amba na
kiambishi cha masharti.
Mfano; Mama
alisema kwamba motto ameumia
Mvulana ambaye ni kaka yangu amerejea nyumbani
Akijua
atanichapa
Vishazi tegemezi vipo vya aina mbili
kutokana na majukumu yake kimuundo
A.
Kishazi tegemezi
kivumishi (bV)
Kishazi tegemezi kivumishi hufanya kazi
ya kuvumisha nomino katika tungo.
Mfano;
Baba anayenijali
Mbwa
aliyepotea
Mwanafunzi
aliyefariki
Uliyemuona pale
Aliyempenda sana
B.
Kishazi
tegemezi kielezi (bE)
Kishazi hiki hufanya kazi ya kueleza tendo
katika tungo na hujitokeza kueleza dhima tofauti tofauti kama ifuatavyo:-
ü Kueleza
mahali tendo linapofanyika. Mfano; Alipoingia
(mahali dhahiri), Alimochungulia (ndani ya kitu Fulani),
Alikoelekea
(mahali pasipo dhahiri)
ü Kueleza
wakati wa tendo. Mfano; Tulipotoka,
Alipomchapa,
Walipomsema
n.k.
ü Kueleza masharti katika tendo. Mfano; Akirudi,
Angekuja,
Angelimpiga,
Angalijua
n.k.
ü Kueleza
namna tendo linavyofanyika. Mfano;
Alivyoimba,
Walivyopendeza,
Tulivyomsifu.
ü Kueleza
kasoro katika kukamilisha tendo.
Mfano; Ingawa amesoma, Licha ya kufaulu, Japokua
amependekezwa.
ü Kueleza
sababu ya kufanyika kwa tendo. Mfano;
Kwa
sababu alipendeza, Kwa kuwa hujafaulu, Kwa
vile umenisomesha.
Je namna ya kutenganisha vishazi huru na tegemezi?????????
JibuFuta